JESHI  la Polisi Mkoani Tanga limefanikiwa kukamata  baadhi ya vitu  vilivyoporwa kufuatia ajali iliyosababisha kifo cha msanii  wa  maigizo na muziki wa kizazi kipya nchini hapa, Hussein Ramadhani Mkiety   maarufu kama Sharo Milionea ambaye alikufa baada ya gari aliyokuwa  akisafiria kuacha njia na kupinduka. 
Kamanda  wa Polisi Mkoa wa  Tanga, Constantine Massawe amesema kuwa vifaa hivyo vimepatikana kumetokana na jeshi la Polisi kufanya msako mkali kwa kushirikiana na  wananchi wa Kijiji cha Songa Maguzoni.
Kamanda Massawe amesema msakohu umefanikiwa kukamatwa kwa  vitu hivyo mbalimbali, zikiwemo nguo alizokuwa amevaa marehemu  Sharomilionea.
Massawe alivitaja miongoni  mwa vitu vilivyokamatwa ni Betri ya gari na Redio ya gari vilikuwa katika gari la marehemuj pamoja na tyrebegi  lililokuwa na nguo alizovuliwa marehemu siku ya ajali ambazo  inadhaniwa kuwa ndizo alizokuwa amezivaa, ikiwemo sambamba na mkanda,suruali na saa  ya mkononi.
Aidha alisema kwamba watuhumiwa walioiba vifaa hivyo  walimtumia mtu mmoja ambaye alikwenda kuvisalimisha kwa Mwenyekiti wa  Serikali ya Kijiji hicho cha songe, Abdi Zawadi ambapo wengine wanaotuhumiwa  kuhusika na wizi huo wakihama kaya zao wamekimbia.
Alisema  kuwa Polisi walifanikiwa kuikamata simu hiyo ya mkononi ya marehemu aina ya  Blackberry ambayo tayari ilikuwa katika mikono ya mnunuzi na  ilishaondolewa chipu kwa lengo la kuuzwa.
“Baada ya kuweka mtego wa kuinunua tumeikuta tayari imeshaondolewa chipu  sasa sijui ilikuwa na hela lakini vitu vingine vimesalimishwa kwa  Mwenyekiti wa Kijiji “,alisema Kamanda huyo.
Hata  hivyo alisema kuwa licha ya watuhumiwa wa wizi huo kufahamika lakini  wamekimbia makazi yao tangu kuanza kwa msako huo na kwamba Jeshi la  Polisi linaendelea kuwatafuta.
Marehemu  Sharo Milionea aliiaga dunia usiku wa kuamkia Novemba 27 mwaka huu  majira ya saa 2.00 usiku eneo la Songa-Maguzoni wilayani Muheza mkoani  Tanga katika barabara Kuu ya Segera kwenda Tanga baaada ya gari  alilokuwa akiendesha kuacha njia na kupinduka.
Sharo Milionea alizikwa Novemba 28 mwaka huu huko Kijijini kwao Lusanga wilaya ya Muheza mkoani Tanga.
credit kwa rockersports
        
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
0 comments :
Speak up your mind
Tell us what you're thinking... !