
MKAZI wa Kijiji cha Kilombero, mkoani Geita, Mahangaiko Buruhe  (52) amefariki dunia baada  ya kusombwa na upepo mkali ulioambatana na  mvua wakati akijaribu kuzuia nyumba yake isianguke.
Tukio hilo lilitokea juzi  saa 10;00 jioni ambapo  marehemu alikuwa akizuia nyumba yake isisombwe na upepo baada ya  kushuhudia paa la nyumba  likiezuliwa na upepo.
Marehemu aliamua kurukia kenchi ili kuzua nyumba isianguke kwa kutumia nguvu zake na kwamba upepo ulimzidi nguvu, paa likaezuliwa na marehemu kurushwa nje na kuangukia nyumba ya pili alikopoteza maisha.
Marehemu aliamua kurukia kenchi ili kuzua nyumba isianguke kwa kutumia nguvu zake na kwamba upepo ulimzidi nguvu, paa likaezuliwa na marehemu kurushwa nje na kuangukia nyumba ya pili alikopoteza maisha.
Mashuhuda wa tukio hilo Makwiwa Bihalale (mke wa  marehemu) na Chausiku Malole walisema marehemu alikuwa akifanya juhudi  za kuokoa nyumba isianguke na upepo ndipo mauti yakamkuta hali ambayo  imewashtua.
Akizungumza mbele ya viongozi waliotembelea hapo  kuona tukio hilo, Kaimu Ofisa Tarafa  ya Busanda, Joseph Kaparatus  alisema tukio hilo lilitokana na ujenzi mbovu wa nyumba hiyo na kwamba  iliezekwa bila kuzingatia utaalamu na haina  kenchi zaidi ya mbao ambazo  zimegongelewa bati.
“Nyumba hii ilikuwa na uhalali wa kuanguka mkuu, angalia haijajengwa kwa kuzingatia utaalamu wa ujenzi wa nyumba,” alisema Kaparatus.
“Nyumba hii ilikuwa na uhalali wa kuanguka mkuu, angalia haijajengwa kwa kuzingatia utaalamu wa ujenzi wa nyumba,” alisema Kaparatus.
Awali akizungumza na wakazi wa eneo hilo nyumbani  kwa marehemu Mkuu wa Wilaya ya Geita, Said Mangochie aliwataka wanachi  hao kujenga nyumba bora zinazozingatia  utaalamu ili kuepusha majanga  wakati wa mvua.
Mwenyekiti wa kijiji hicho Haruna Shabani alisema  marehemu aliwahi kuwa mtendaji wa kijiji, na kiongozi wa CCM Kata ya  Busanda, ameacha wajane wawili na watoto 18.
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
