Wema Sepetu Mwigizaji bora wa kike Swahiliwood.
KILA Siku tasnia ya filamu Swahiliwood inazidi kupiga hatua na  kujikuta kuna mambo yanayopaswa kuainishwa kwa wapenzi wa filamu na  wadau kwa ujumla wake, tasnia ya filamu ni pana lakini kuna maeneo  yanayogusa tasnia hiyo kwa ujumla wake ni waigizaji, leo tuangalia  wasanii kumi bora wanaongoza kwa mauzo.
Wema Sepetu mkali wa filamu Sawhiliwood.
1. Marehemu Steven Kanumba pamoja na kutokuwepo hai baada ya mwaka  mmoja kuondoka Duniani ameonekana kuwa ndio kinara wa mauzo hadi sasa  msanii huyo ambaye amekuwa akishindana na swahiba yake Ray mauzo yake  yalipanda baada ya kifo chake kuanzia mwezi wa Tano mwaka 2012.
.
.
Kanumba amerudi tena mwezi wa nne kwa kuvunja rekodi ya mauzo ya  filamu baada ya filamu yake ya Love and Power kuingia sokoni filamu hiyo  inampa nafasi hayati Kanumba kushika namba ya kwanza Bongo.
Nambari mbili inakwenda kwa Vincent Kigosi msanii ambaye
inasemekana kuwa toka kuanza kwake kuigiza na kuwa mtayarishaji wa  filamu kazi zake hazijawahi kuyumba sokoni na kuwatia hasara wasambazaji  kwani kazi zake hazidodi, Ray filamu ambazo zinampatia nafasi ya pili  ni filamu ya Women of Princeple, waves of sorrow. Imemfanya azidi  kupanda na kuwa juu.
Namba hii inawakutanisha wasanii wawili kwa mpigo Jacob Stephen ‘JB’  na Amri Athuman ‘King Majuto’ hawa wameweza kushiriki katika filamu  nyingi lakini filamu iliyoweza kuwapa nafasi ya tatu ni Nakwenda kwa  Mwanangu filamu iliuza sana.JB amekuwa ni mwigizaji wa kipekee kwa muda  sasa huku King Majuto aking’ara katika vichekesho na filamu pia.
Namba hiyo pia kuna wasanii wanagongana na na kuibuka nafasi hiyo  wasanii hao ni Hashim Kambi, Haji Salum ‘Mboto’ Hashim Kambi amekuwa  mahiri hadi hivi karibuni alichukuliwa na kwenda kuigiza nchini Ghana,  wakati Mboto ndio msanii pekee ambaye amekuwa akiigiza kama mchekeshaji  pekee anayeigiza filamu kama Fall in Love, Nampenda mke wangu, Redio  Presenter .
Yusuf Mlela kijana anayefanya vema katika tasnia ya filamu toka  kuingia kwake katika filamu, msanii Mlela filamu zake kama Poor mind,  Nifute Machozi zinampa nafasi hiyo nakuwa msanii bora namba tano.
Hao walikuwa wasanii bora wa kiume ambao wanafanya vizuri katika  tasnia ya filamu toka mwezi January hadi mwezi May ukija kwa upande wa  akina dada mwanadada Wema sepetu ndio nambari moja yaani Bora kwa  wasanii wa kike pamoja kushiriki chache lakini ndio kinara,filamu 14  Days, It was not me, Dj Ben.
.
.
Namba mbili Inakwenda kwa mwanadada nyota Jacqueline Wolper naye  kashiriki filamu nyingi lakini filamu ambayo wengi wanamuongelea ni  Dreva Taxi .
Namba tatu Riyama Ali mwigizaji bingwa katika maisha ya kila aina  anakuwa ni msanii mwenye kuvaa husika kwa filamu zenye huzuni, msanii  ambaye ni mkongwe aliwahi kuibuka msanii bora kupitia filamu ya Fungu la  Kukosa 2005/2006 Riyama msanii filamu zake ni Tabu ya kuoleana, Best  wife, The Dream zimemng’arisha.
4. Jennifer Kyaka mwigizaji ambaye pia ni mtayarishaji wa filamu kwa  kampuni yake ni mwigizaji ambaye anastaili kuingia na kushika nafasi ya  nne filamu zinazompatia nafasi hiyo ni Rude, Pain killer.
5. Nambari hiyo inawakutanisha wasanii wawili ambao ni Aunt Ezekiel,  na Ruth Suka ,Mainda , Aunty baada ya kushiriki kama I hate my birthday  na nyinginezo anaibuka kwa kushiriki na filamu zake anazoshirikisha  komediani filamu kama Nampenda mke wangu Radio Presenter na zingine,  mainda anafanya vema na filamu ya Rude.
Hiyo ndio kumi bora katika tasnia ya filamu Swahiliwood inayofanya  vizuri kwa sasa kuanzia mwaka jana hadi leo, utafiti huu kwa mujibu wa  filamucentral.
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
0 comments :
Speak up your mind
Tell us what you're thinking... !